Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

14 Januari 2021

Hii leo jaridani kwa kiasi kikubwa ni masuala ya mabadiliko ya tabianchi tukimulika ripoti ya shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP, kuhusu hatua thabiti za kuhimili mabadiliko ya tabianchi na kutumia mbinu za asili, halikadhalika ripoti kuhusu viwango vya joto kutoka shirika la hali ya hewa la Umoja wa Mataifa, WMO, ikiutaja mwaka 2020 kuwa moja ya miaka mitatu iliyoongoza kwa kuwa na viwango vya juu sana vya joto duniani. Tunakwenda pia huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR ambako mapigano mapya yamesababisha vikosi vya walinda amani wa Umoja wa Mataifa kuchukua hatua.

Sauti
10'53"