Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

FAO/Rudolf Hahn

Mabadiliko ya tabianchi, tishio kwa eneo la bonde la ufa Kenya

Kuongezeka kwa maji kwenye maziwa yaliyo eneo la bonde la ufa nchini Kenya ni jambo ambalo linaendelea kuzua wasiwasi miongoni mwa watu wa maeneo hayo na pia pigo kubwa kwa sekta muhimu ya utalii nchini Kenya. Serikali imekuwa ikiwashauri wale wanaoishi karibu na maeneo hayo kuhama na kujitafutia sehemu salama huku ikitafuta suluhusu ikiwa maji hayo yatazidi kuongezeka siku zinazokuja. Mwandishi wa Kenya Jason Nyakundi amezungumza na mtaalamu wa hali ya hewa nchini Kenya Henry Ndede kutaka kufahamu chanzo ni kipi.

Sauti
2'38"