Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mkutano wa 26 wa kimataifa wa mbadiliko ya tabianchi COP26 uliokuwa ufanyike baadaye mwaka huu umehairishwa.
Unsplash/Adam Marikar

Mkutano wa mabadiliko ya tabianchi umeishaje, na nini kinafuata?

Wakuu wa nchi na serikali zaidi ya 70 , wakiwemo pia viongozi wa kikanda, mameya wa miji mbalimbali na wakuu wa mashirika mbalimbali duniani wamewasilisha hatua wanazotarajia kuchukua ili kupunguza kiwango cha hewa chafuzi ya viwandani na kuzuia dunia kuendelea kuchemka na ongezeko la joto katika mkutano wa matamanio ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi uliomalizika Jumamosi jioni.