Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Moshi kutoka kwa nyumba ya kuoka mikate inayotumia mkaa.
UNICEF/Shehzad Noorani

Kupungua kwa hewa chafuzi angani kunaweza kusaidia kufikia lengo la chini ya nyuzi joto 2 za Selisiasi-UNEP 

Janga la uchafuzi wa hali ya hewa linaweza kupungua hadi asilimia 25 kwenye uzalishaji wa hewa chafuzi uliotabiriwa kufikia mwaka 2030 na hivyo kuileta dunia karibu kufikia lengo la nyuzi joto 2 kipimo cha selisiasi za Mkataba wa Paris, imeeleza ripoti mpya ya shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP.