Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN Photo/David Mutua

Dunia inahitaji kuchukua hatua zaidi kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi-UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, kesho Jumatano likifanya mkutano wa ngazi ya juu kushughulikia athari za mabadiliko ya tabianchi kwa wakimbizi na wakimbizi wa ndani, pamoja na wengine walio katika mazingira hatarishi kote, mshauri maalumu wa UNHCR kuhusu mabadiliko ya tabianchi Andrew Harper amesema dunia inapaswa kuchukua hatua kali zaidi kwani mabadiliko ya tabia nchi huwezi kuyavalia barakoa. 

Sauti
1'49"