Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

World Bank/Sue Pleming

Hali ya hewa ya Morogoro haikuwa hivi, hatua za pamoja na za haraka zinahitajika-Wakazi wa Morogogo

Mkoa wa Morogogoro ulioko katika eneo la mashariki la Tanzania ni moja ya maeneo ambayo kwa miaka mingi yametambulika kuwa maeneo yenye hali nzuri ya hewa kutokana na mazingira yake kuwa yenye misitu, nyika, na milima yenye kutiririsha maji safi. Lakini katika miaka ya hivi karibuni wanaharakati wa kutunza mazingira wanaona kuwa ni muhimu kuchukua hatua za kuilinda hali hiyo kwani iko katika hatari ya kutoweka kutokana na shughuli za binadamu kama vile uchomaji mkaa.

Sauti
3'36"

05 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Assumpta Massoi 
-Lebanon,iko katika siku ya maombolezo kufuatia mlipuko mkubwa wa jana katika mji mkuu Beirut UNIFIL iko tayari kusaidia.
 - Nchini Niger, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linashirikiana na wadau kutekeleza mbinu za haraka za kukabiliana na utapiamlo uliokithiri miongoni mwa watoto .
- Takwimu za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR zinaonesha kuwa theluthi mbili ya raia milioni mbili wa Sudan Kusini wanaoishi uhamishoni, ni watoto.

-Na le

Sauti
11'52"