Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN News/Assumpta Massoi

Wananchi wanaelewa kuhusu mabadiliko ya tabianchi baada ya kuiona hali halisi

 Mafuriko, mvua za kupindukia, ukame na kuyeyuka kwa barafu ni ishara kubwa ya mabadiliko ya tabianchi lakini ni hadi wakazi wa ulimwengu wayashuhudie ndipo wanaamini, hivyo ndivyo anavyoeleza Kaimu Afisa Mazingira wa wilaya ya Pangani katika mahojiano na Saa Zumo wa Redio washirika Pangani FM, kuhusu hatua na harakati zinazofanywa na mamlaka ya wilaya ya Pangani katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

 
 
 
 
 
 
Sauti
2'19"

27 APRILI 2020

Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea 

-Watoto wengi wakosa chanjo hata kabla ya  kuzunga kwa janga la virusi vya Corona au COVID-19 limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF likitaka hatua madhubuti zichukuliwe sasa kuhakikia watoto wanapata chanjo zote

-Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF leo limeanza kusambaza mashine za hewa ya Oxygen katika vituo sita vya afya vinavyohudumia wagonjwa wa COVID-19

Sauti
11'