Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN News/Assumpta Massoi

Mabadiliko ya tabianchi Pangani, Tanga ni dhahiri- Afisa Mifugo

Kadri siku zinavyosonga hivi sasa, shughuli za binadamu zinavyoshamiri, vivyo hivyo mabadiliko ya tabianchi ambayo nayo yanazidi kuwa dhahiri miongoni mwa wakazi wa maeneo mbalimbali. Kila sekta imeguswa. Hali inakuwa ni changamoto zaidi kwa wakazi walio karibu na fukwe au wanaopakana na bahari. Mathalani nchini Tanzania kwa wakazi wa Pangani mkoani Tanga shughuli za kilimo,uvuvi na ufugaji zimeathirika na wanapaswa kuchukua hatua zaidi. Je madhara ni kwa kiasi gani?

Sauti
4'26"