Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN News/ John Kibego

Nyasi vamizi zageuka fursa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi nchini Uganda

Mabadiliko ya tabianchi yanazidi kusababisha wasiwasi miongoni mwa jamii za wafugaji Afrika na kwingineko ulimwenguni hasa kutokana ukame wa muda mrefu. Hata hivyo, nchini Uganda hatua zinachukuliwa ambapo wameanza kubaini nyasi zinazoweza kuhiili mabadiliko haya ya tabianchi na hatimaye kuzihamishia katika maeneo mbalimbali ya nchi ili ziwasaidie badala ya kutegemea malisho asilia katika eneo fulani.

Mmoja wa wale ambao wamevalia suala hilo njuga ni Mbunge wa Kaunti ya Butemba wilaya ya Kyankwanzi Innocent Pentagon Kamusiime ambaye amepanda nyasi aina ya  Kikuyu.

Sauti
3'42"