Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN News/Assumpta Massoi

Je wajua kuwa ukubwa wa ziwa Tanganyika unazidi kupungua?

Nchini Tanzania, Ziwa Tanganyika lililopo mkoani Kigoma lasifika kwa kuwa la pili kwa kuwa na kina kikubwa zaidi duniani. Hata hivyo, kina na ukubwa wa ziwa vinapungua kutokana na mabadiliko ya tabianchi na shughuli za binadamu. Miongoni mwa mashuhuda wa hali hiyo ni Bwana  Kassim Govola Mbingo ambaye ni mhifadhi mkuu katika makumbusho ya Dkt. David Livingstone mjini Ujiji mkoani Kigoma. Katika mahojiano yake na Assumpta Massoi wa Idhaa hii ya Kiswahili ya  Umoja wa Mataifa anafafanua

Sauti
3'55"

13 JANUARI 2020

Katika Jarida la Habari hii leo Grace Kaneiya anakuletea

-Miaka 10 baada ya tetemeko baya la ardhi nchini Haiti athari zake zinaendelea kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM

-Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeutenga mwaka 2020 kuwa ni wa afya ya mimea kwa kutambua mchango na thamani ya mimea hiyo kwa maisha ya watu na syari dunia

-Maelfu ya Wavenezuela wakiwemo watoto wanaendelea kufungasha virago na kukimbilia nchi jirani ikiwemo Brazil limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF

Sauti
11'50"