Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu
Greta Thunberg ahoji uthubutu wa viongozi kusalia na maneno huku watu wakipoteza maisha
Leo katika ufunguzi wa mkutano wa ngazi ya juu wa viongozi wa Umoja wa Mataifa kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Gutrerres amesema hatakuwa mtamazaji aliye kimya kwa uhalifu ambao unaathiri hali ya sasa na kuharibu haki kwa vizazi vijavyo kwa ajili ya mustakabali endelevu akiongeza kwamba viongozi wana haki ya kufanya kila wawezalo kukomesha janga la mabadiliko ya tabianchi kabla halijatukomesha.
Miji kote ulimwenguni ni ‘sababu kuu ya mabadiliko tabianchi’- UN-Habitat
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la makazi la Umoja wa Mataifa UN-Habitat Maimunah Mohd Sharif, miji kote ulimwenguni ni ‘sababu kuu ya mabadiliko tabianchi’ ingawa pia inaweza kuwa na suluhisho la kupunguza hewa chafuzi gesi, ambazo zinasababisha joto ulimwenguni kuongezeka.