Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu
Tunahitaji kukomesha mabadiliko ya tabianchi:UN
Tunahitaji kuhakikisha tunakomesha mabadiliko ya tabianchi amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres baada ya kurejea kutoka Abaco katika visiwa vya Bahama ambako kumeathirika sana na kimbinga doriani.
Shmbulio dhidi ya kituo cha mafuta Saudia linatutia hofu:Griffiths
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen Martin Griffiths amesema anatiwa hofu kubwa kuhusu mashambulio yaliyofanywa na ndege isiyo na rubani au drine katika vituo viwili vya mafuta kwenye Ufalme wa Saudi Arabia.
Akizuru visiwa vya Bahama Guterres ataka hatua zaidi dhidi ya mabadiliko ya tabianchi
Viongozi wa dunia watakaohudhuria mkutano unaokuja wa hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa wametakiwa kuja wamejizatiti sio na hotuba bali mipango ya kufikia malengo ya kupunguza hewa ukaa na kuimarisha mnepo dhidi ya changamoto hiyo ya kimataifa.