Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mabadiliko ya tabianchi na matumizi mabaya ya ardhi yamechangia katika kusababisha jangwa kwa mfano katika eneo la kaskazini mashariki mwa Cameroon (Januari 2019)
UN News/Daniel Dickinson

Rejesha ardhi katika ubora wake ili kuiokoa dunia na kukuza uchumi- Ibrahim Thiaw

Mkutano wa 14 wa nchi wanachama wa mkataba wa kuzuia kuenea kwa jangwa, UNCCD ukiendelea huko  New Delhi, India, Katibu Mtendaji wa mkataba huo Ibrahim Thiaw amesema  dunia sasa inatakiwa kuwekeza katika urejeshaji wa ardhi katika ubora kama njia mojawapo ya kuboresha ustawi wa maisha, kupunguza hatari za mabadiliko ya tabianchi  na kupunguza hatarizinazoweza kuyumbisha uchumi.