Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres (Kulia) na mwenyekiti wa tume ya Muungano wa Afrika Moussa Faki Mahamat wakihutubia waandishi wa habari.
Video Screen Shot

Kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, usalama na amani ni muhimu katika kufikia maendeleo Afrika-AU, UN

Mabadiliko ya tabianchi ni moja ya masuala ambayo yataathiri ukuaji wa uchumi wa bara Afrika iwapo uchafuzi wa mazingira hautapunguzwa kwa asilimia 45 kufikia mwaka 2030 na kutokomezwa kabisa ifikapo mwaka 2050 amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihutubia waandishi wa habari Jumatatu alasiri jijini New York, Marekani.