Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN News/ Anton Uspensky

Athari za mabadiliko ya tabianchi hazina mipaka- mkaazi Bunyoro-Uganda

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linachagiza mataifa kuchukua hatua za haraka ambazo zinaweza kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Lengo hilo limeorodhesha malengo madogo ambayo yatasaidia katika kufanikisha SDG 13 ifikapo mwaka 2030. Katika kupima utekelezaji wa lengo hilo, moja ya hatua ni kuimarisha uwezo wa kupanga na kusimamia mbinu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika nchi maskini, visiwa vidogo na zile zinazoendelea, ikiwemo kwa kulenga wanawake,vijana na jamii mashinani na zilizotengwa.

Sauti
3'41"