Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Kimbunga Hagupit kilipopiga Ufilipino tarehe 5-6 Desemba 2014, hali ilikuwa mbaya kwani nchi  hiyo bado ilikuwa haijasahau madhara ya kimbunga Haiyan kilichotokea Novemba 2013.
OCHA/Jennifer Bose

Mamia wakielekea Marrakech, CO24 nayo yajadili tabianchi na uhamiaji

Wakati mamia ya watunga sera wakikusanyika huko Marrakech nchini Morocco kwa ajili ya kukubaliana juu ya mkataba mpya wa kimataifa kuhusu uhamiaji, mkutano wa 24 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP24 huko Katowice Poland, nao unajikita katika njia thabiti za kusaidia nchi kukabiliana na ukimbizi wa ndani  utokanao na madhara ya mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ukosefu wa maji, mafuriko, vimbunga na kuongezeka kwa kina cha maji ya bahari