Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

IFAD

Sasa ufuta tunavuna, tunakula na tunauza shukrani IFAD- Wakulima Chad

Nchini Chad mradi wa mfumo wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo, IFAD umesaidia wakulima kukabiliana na matatizo yaliyowakumba katika kilimo cha zao la ufuta linalotegemewa kwa lishe na kipato. 

Ndani ya nyumba ya mkulima mmoja nchini Chad, anaonekana Pierre Thaim, balozi huyu wa mapishi ya Afrika kutoka New York, Marekani akiwa amemtembelea mkulima wa ufuta Fatime Saleh ili kujionea jinsi mabadiliko ya tabianchi yaliyoathiri kilimo cha zao hili. Kwa pamoja wanasaidiana kusagisha ufuta, kiambato muhimu kwa mlo kwenye nchi hii ya Afrika Magharibi.

Sauti
1'50"