Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN Photo/Sophia Paris

Taka zaepusha matumizi ya dizeli Uganda

Matumizi ya nishati mbadala na salama ni jambo ambalo linapigiwa chepuo na Umoja wa Mataifa ambapo lengo namba 7 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linasisitiza nishati rahisi na salama. Hatua hii inazingatia kwamba idadi ya watu wanaohitaji nishati ya umeme inaongezeka kila siku na hivyo kutoa changamoto ya kusaka vyanzo mbadala vya nishati kwani umeme pekee uliozoeleka ni wa vyanzo vya maji, na ukame unatishia uwepo wa mabwawa ya maji. Ni kwa kuzingatia hilo huko Uganda, wanatumia mabaki ya taka au biomasi ili kuzalisha nishati. Je nini kinafanyika?

Sauti
3'16"