Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mwaka mmoja wa mkataba wa Paris, mafanikio ni dhahiri

Mkutano wenye lengo la kuchagiza utekelezaji wa mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi utafanyika kesho mjini Paris, Ufaransa, ukienda sambamba na maadhimisho ya mwaka mmoja tangu kutiwa saini kwa nyaraka hiyo.

Viongozi wa ngazi ya juu watashiriki mkutano huo akiwemo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António  Guterres, Rais wa benki ya Dunia pamoja na mwenyeji wao Rais wa Ufaransa.

Wakati wa mkutano huo, hatua zinazochukuliwa za kufanikisha mkataba huo zitawekwa bayana ikiwemo hatua za nchi kukabili mabadiliko ya tabianchi.