Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Joto na mafuriko huathiri wanawake na wanaume wa vijijini tofauti na kuongeza tofauti ya kipato
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limezitaka nchi kuhakikisha zinashughulikia changamoto za usawa wa kijinsia kwenye kupambana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwani takwimu zinaonesha kuwa familia hususan za vijijini zinazoongozwa na wanawake zinaathirika zaidi na mabadiliko ya tabianchi ikilinganishwa na zile zinazoongozwa na wanaume.
Mkuu wa UN aomba msaada zaidi kwa visiwa vidogo vinavyopambana na mabadiliko ya tabianchi
Ufadhili zaidi unahitajika kusaidia nchi zinazoendelea za visiwa vidogo SIDS, vilivyo katika mstari wa mbele wa mabadiliko ya tabianchi, amesema Jumamosi Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiwa katika visiwa vya Saint Vincent na Grenada.
Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa ni nini na kwa nini ni muhimu?
Umewadia wakati ambapo nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa zitapata fursa ya kuonesha kwamba vitendo vya mazingira vinaweza kuunganisha ulimwengu. Wakati huu ni Baraza la Umoja wa Mataifa la Mazingira, au Unea, ambalo mkutano wake wa sita utafanyika kati ya Februari 26 na Machi 1, 2024 Nairobi, Kenya.
Mkutano wa Baraza la Mazingira Duniani UNEA6 wangoa nanga Nairobi Kenya
Mkutano wa sita wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEA6 leo umefungua pazia katika Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo jijini Nairobi, nchini Kenya. Mkutano huo utakaodumu kwa siku tano unahudhuriwa na washiriki zaidi ya 6000 ikiwa ni pamoja na viongozi wa Mazingira duniani, asasi za kiraia, wataalamu wa Mazingira, maofisa waserikali za mitaa, wakulima, vyama vinavyowakilisha wafanyakazi, jamii zilizoachwa nyuma pamoja na maofisa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa.
Tuangalie mtindo mpya wa ufadhili kwa wakulima na wafugaji waathirika wa mizozo - FAO
Takriban watu milioni 258 katika nchi na maeneo 58 ulimwenguni wanakabiliwa na njaa kali inayochochewa na migogoro ya silaha, majanga ya kiuchumi, mabadiliko ya tabianchi, umaskini na ukosefu wa usawa, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na kutaka wadau kuangalia upya mtindo wa ufadhili.
FAO yasihi wadau kuangalia mtindo mpya wa ufadhili
Takriban watu milioni 258 katika nchi na maeneo 58 ulimwenguni wanakabiliwa na njaa kali inayochochewa na migogoro ya silaha, majanga ya kiuchumi, mabadiliko ya tabianchi, umaskini na ukosefu wa usawa, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na kutaka wadau kuangalia upya mtindo wa ufadhili.
Mwanafunzi Msumbiji: Iwe mvua iwe upepo mkali madarasa yetu ni salama
Kila mwaka, Msumbiji hukabiliwa na matukio ya hali mbaya za hewa kupindukia kama vile vimbunga na mafuriko, matukio ambayo husababisha uharibifu wa shule na hatimaye watoto kushindwa kujifunza. Hata hivyo, ujenzi wa madarasa yanayohimili matukio kama vile pepo kali na mafuriko umeleta nuru na matumiani kwa watoto, wazazi na walimu. Madarasa haya yanawezesha watoto kubakia salama hata wakati wa mvua na upepo mkali. Hali hii ni uwekezaji wa kudumu kwani ni hakikisho kwa watoto kuendelea kupata elimu na mustakabali wao kuwa bora.
Mwaka 2024 tishio kwa watoto: Ripoti ya UNICEF
Duniani kote mwaka 2024, watoto wanatarajiwa kuona kuongezeka kwa matukio ya ghasia, vita na matatizo ya kiuchumi, linasema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF), katika utafiti uliotolewa siku ya Jumatatu ya Januari 15, 2024.
Guterres: Vita, mabadiliko ya tabianchi na AI ni changamoto tunazopaswa kuzishughulikia haraka
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo amehutubia jukwaa la uchumi duniani mjini Davos Uswis akigusia changamoto mbalimbali zinazpoikabili dunia hivi sasa kuanzia vita inayoendelea Gaza na kwingineko, hali ya kutochukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na maendeleo ya akili mnemba au AI.