Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA
Lugha ya kiswahili kuadhimishwa kimataifa kila tarehe 7 Julai - UNESCO

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO tarehe 23 mwezi Novemba mwaka 2021 lilitangaza rasmi tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Maudhui ya maadhimisho ya mwaka huu ni Kiswahili kwa amani na ustawi. Lengo hasa la maadhimisho haya ya mwaka ni kusongesha matumizi ya lugha ya kiswahili kama nguzo ya amani, na ustawi na wakati huo kuimarisha tamaduni mbalimbali.

UNESCO ilipitisha uamuzi huo huko makao makuu yake mjini Paris Ufaransa wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa shirika hilo.
Azimio lilipitishwa bila kupingwa na utekelezaji wake unaanza mwaka huu wa 2022.

Kupitia ukurasa huu mahsusi, utapataa taarifa zote kuanzia kupitishwa kwa azimio hilo, mapokeo yake na harakati za kukuza lugha ya Kiswahili ili iweze kujenga amani, uchumi, maendeleo na utangamano katika kona mbali mbali za dunia.

Utapata taarifa zilizochapishwa, video kutoka watu mbalimbali iwe maafisa wa serikali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, maafisa wa UN wenyewe, wanazuoni, wanafunzi na wananchi wa kawaida.


 

Mapigano yasitishwa mji mkuu Sana’a na sasa yahamia viungani

Nchini Yemen baada ya mfululizo wa mashambulizi ya anga na ardhini kuanzia mwishoni mwa wiki kwenye mji mkuu Sana’a, hatimaye hii leo mashambulizi yamekoma na hivyo wananchi kuweza kuibuka kutoka kwenye makazi yao ili kupata huduma.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka mjini humo, mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen, Jamie McGoldrick amesema siku tano za machungu zimekoma baada ya kusabaisha vifo vya watu wapatao 125 na mamia ya majeruhi.

WHO yatoa msaada wa vifaa vya tiba Libya

Shirika la afya duniani  WHO limetoa msaada wa mitambo ya kusaidia kupumua kwa wangonjwa mahututi katika hospitali ya Tragen kusini mwa Libya

Msaada huo wa mitambo miwili pamoja na vipuri vyake vyote umetolewa kufuatia kuwepo na upungufu mkubwa wa vifaa hivyo vya tiba kwa wagonjwa mahututi na wenye kuhitaji usaidizi wa kupumua.

WHO imeeleza kujizatiti kuendelea kutoa msaada wa kibinadamu kwenye nyanja ya afya maeneo yote nchini Libya .

Fedha za kununulia vifaa tiba hivyo zimetoka kwenye mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa CERF

Saidieni kupambana na uharibifu wa mazingira: Guterres

Tuna haki ya kuishi sehemu salama, tunategemea kula chakula bora, maji safi na kuvuta hewa safi lakini bado tunaendelea kuharibu mazingira.

Huo ni ujumbe wa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika mkutano mkuu wa shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa unaofanyika Nairobi, Kenya.

Guterres amesema tayari kuna mbinu na maazimio madhubuti za kupambana na mabadiliko ya tabia nchi yanayoweza kuigwa kuinusuru dunia isiendelee kuathirika.

Tuwe makini maendeleo yasisababishe zahma- Lajčák

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Miroslav Lajčák aliyeko ziarani nchini Kenya, amesema maendeleo hayapaswi kusababisha uharibifu wa mazingira.

Amesema hayo jijini Nairobi, wakati akifunga mjadala kuhusu sayansi, sera na biashara, mjadala uliofanyika kwa siku mbili.

Bwana Lajčák amesema hayo akizingatia kuwa harakati za sasa za maendeleo duniani zimekumbwa na vikwazo kama vile majanga ya asili na yale yanayosabishwa na binadamu ambavyo vyote vinatishia siyo tu uwepo wa binadamu bali pia sayari dunia.