Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA
Lugha ya kiswahili kuadhimishwa kimataifa kila tarehe 7 Julai - UNESCO

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO tarehe 23 mwezi Novemba mwaka 2021 lilitangaza rasmi tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Maudhui ya maadhimisho ya mwaka huu ni Kiswahili kwa amani na ustawi. Lengo hasa la maadhimisho haya ya mwaka ni kusongesha matumizi ya lugha ya kiswahili kama nguzo ya amani, na ustawi na wakati huo kuimarisha tamaduni mbalimbali.

UNESCO ilipitisha uamuzi huo huko makao makuu yake mjini Paris Ufaransa wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa shirika hilo.
Azimio lilipitishwa bila kupingwa na utekelezaji wake unaanza mwaka huu wa 2022.

Kupitia ukurasa huu mahsusi, utapataa taarifa zote kuanzia kupitishwa kwa azimio hilo, mapokeo yake na harakati za kukuza lugha ya Kiswahili ili iweze kujenga amani, uchumi, maendeleo na utangamano katika kona mbali mbali za dunia.

Utapata taarifa zilizochapishwa, video kutoka watu mbalimbali iwe maafisa wa serikali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, maafisa wa UN wenyewe, wanazuoni, wanafunzi na wananchi wa kawaida.


 

Guterres alaani mashambulizi ya kigaidi Baghdad leo

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali mashambulizi mawili ya kigaidi yaliyoptokea leo mjini Baghdad nchini Iraq.

Kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Katibu Mkuu ametuma salamu za rambirambi kwa familia za waathirika wa mashambulizi hayo na kuwatakia ahuweni ya haraka majeruhi. Watu zaidi ya 20 wamedaiwa kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa.

Guterres amerejea kusema kwamba Umoja wa Mataifa utaendelea kushikamana na serikali na watu wa Iraq katika juhudi za kupambana na ugaidi na kulijenga upya taifa hilo.