Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA
Lugha ya kiswahili kuadhimishwa kimataifa kila tarehe 7 Julai - UNESCO

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO tarehe 23 mwezi Novemba mwaka 2021 lilitangaza rasmi tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Maudhui ya maadhimisho ya mwaka huu ni Kiswahili kwa amani na ustawi. Lengo hasa la maadhimisho haya ya mwaka ni kusongesha matumizi ya lugha ya kiswahili kama nguzo ya amani, na ustawi na wakati huo kuimarisha tamaduni mbalimbali.

UNESCO ilipitisha uamuzi huo huko makao makuu yake mjini Paris Ufaransa wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa shirika hilo.
Azimio lilipitishwa bila kupingwa na utekelezaji wake unaanza mwaka huu wa 2022.

Kupitia ukurasa huu mahsusi, utapataa taarifa zote kuanzia kupitishwa kwa azimio hilo, mapokeo yake na harakati za kukuza lugha ya Kiswahili ili iweze kujenga amani, uchumi, maendeleo na utangamano katika kona mbali mbali za dunia.

Utapata taarifa zilizochapishwa, video kutoka watu mbalimbali iwe maafisa wa serikali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, maafisa wa UN wenyewe, wanazuoni, wanafunzi na wananchi wa kawaida.


 

Watoto warohigya waliosalia Myanmar wanaishi maisha dhalili- UNICEF

Kitendo cha kushindwa kuwafikia watoto wa kabila la Rohingya ambao bado wamesalia nchini Myanmar kinatutia shaka kubwa kwa kuwa wanaishi kwenye mazingira ya kusitikisha.

Limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF hii leo kufuatia ziara ya msemaji wake huko jimbo la Rakhine nchini Myanmar hivi karibuni.

Marixie Mercado amesema watoto wapatao 60,000 wamenasa kwenye kambi dhalili katikati mwa jimbo hilo la Rakhine wakiwa katika hali mbaya huku ulimwengu ukielekeza zaidi usaidizi wake kwa wakimbizi 655,000 ambao wameingia Bangladesh.

IOM na Zambia wajenga kituo cha mpito kwa wasaka hifadhi mpakani

Nchini Zambia, shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM kwa kushirikiana na serikali wanajenga kituo cha kuhifadhi wahamiaji walio hatarini zaidi kwenye mpaka wa nchi hiyo na Namibia.

Kituo hicho kitapokea wahamiaji na kuwapatia hudukma muhimu kama vile za afya wakati wakisubiri kurejea nyumbani.

Miongoni mwa wahamiaji hao ni wale wanaokuwa wamenusurika kwenye biashara haramu ya binadamu, wasaka hifadhi, wakimbizi na wengineo wanaokimbia hali ngumu ya maisha inayotokana na sababu nyingi ikiwemo majanga ya asili.