Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA
Lugha ya kiswahili kuadhimishwa kimataifa kila tarehe 7 Julai - UNESCO

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO tarehe 23 mwezi Novemba mwaka 2021 lilitangaza rasmi tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Maudhui ya maadhimisho ya mwaka huu ni Kiswahili kwa amani na ustawi. Lengo hasa la maadhimisho haya ya mwaka ni kusongesha matumizi ya lugha ya kiswahili kama nguzo ya amani, na ustawi na wakati huo kuimarisha tamaduni mbalimbali.

UNESCO ilipitisha uamuzi huo huko makao makuu yake mjini Paris Ufaransa wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa shirika hilo.
Azimio lilipitishwa bila kupingwa na utekelezaji wake unaanza mwaka huu wa 2022.

Kupitia ukurasa huu mahsusi, utapataa taarifa zote kuanzia kupitishwa kwa azimio hilo, mapokeo yake na harakati za kukuza lugha ya Kiswahili ili iweze kujenga amani, uchumi, maendeleo na utangamano katika kona mbali mbali za dunia.

Utapata taarifa zilizochapishwa, video kutoka watu mbalimbali iwe maafisa wa serikali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, maafisa wa UN wenyewe, wanazuoni, wanafunzi na wananchi wa kawaida.


 

ICTY muasisi wa haki duniani- Guterres

Hatimaye mahakama ya kimataifa iliyokuwa inaendesha kesi za uhalifu uliofanyika kwenye iliyokuwa Yugoslavia, imefunga pazia rasmi leo baada ya kuhudumi kwa miaka 24.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza huko The Hague, Uholanzi hii leo wakati wa hitimisho la ICTY, ameielezea kuwa ni muasisi wa haki ya kimataifa.

Katika kipindi cha uwepo wake, ICTY imehukumu watu 90 kwa uhalifu waliotenda huko Yugoslavia ikiwemo mauaji ya kimbari, uhalifu wa kivita na uhalifu wa kibinadamu wakati wa vita vya Balkan miaka ya 90.

Dola Milioni 105 kunufaisha Mama na Mtoto Msumbiji

Huduma ya msingi ya afya kwa mama na mtoto sasa itaimarika nchini Msumbiji baada ya Benki ya dunia kuidhinisha dola Milioni 105 kwa ajili ya kuipa serikali ya nchi hiyo.

Msaada huo wa kifedha unafuatia programu maalum ya miaka mitano iliyoanzishwa na Msumbiji kwa ajili ya kuwezesha kuboresha huduma za afya ambazo kwa sasa viko chini sana kwa mujibu wa viwango vya maendeleo ya binadamu vikishika nafasi ya 181 kati ya 188