Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA

LUGHA YA KISWAHILI KIMATAIFA
Lugha ya kiswahili kuadhimishwa kimataifa kila tarehe 7 Julai - UNESCO

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO tarehe 23 mwezi Novemba mwaka 2021 lilitangaza rasmi tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Maudhui ya maadhimisho ya mwaka huu ni Kiswahili kwa amani na ustawi. Lengo hasa la maadhimisho haya ya mwaka ni kusongesha matumizi ya lugha ya kiswahili kama nguzo ya amani, na ustawi na wakati huo kuimarisha tamaduni mbalimbali.

UNESCO ilipitisha uamuzi huo huko makao makuu yake mjini Paris Ufaransa wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa shirika hilo.
Azimio lilipitishwa bila kupingwa na utekelezaji wake unaanza mwaka huu wa 2022.

Kupitia ukurasa huu mahsusi, utapataa taarifa zote kuanzia kupitishwa kwa azimio hilo, mapokeo yake na harakati za kukuza lugha ya Kiswahili ili iweze kujenga amani, uchumi, maendeleo na utangamano katika kona mbali mbali za dunia.

Utapata taarifa zilizochapishwa, video kutoka watu mbalimbali iwe maafisa wa serikali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, maafisa wa UN wenyewe, wanazuoni, wanafunzi na wananchi wa kawaida.


 

Watoto wa kike wang’ara utafiti wa kujua kusoma- UNESCO

Zaidi ya asilimia 96 ya watoto wenye umri wa miaka ya kati ya 9 hadi 10 wanajua kusoma

Ripoti ya utafiti wa zaidi ya nchi 50 duniani uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO umeonyesha kuwa watoto wa kike wanaongoza zaidi kuliko wa kiume.

Nchi ya Urusi imeongoza katika utafiti huo ikifuatiwa na Singapore, Hong Kong, Ireland, Finland na Poland.

Utafiti huo uliofanywa na wataalamu wa UNESCO  kwa kushirikiana na wadau wengine wa elimu ni wa kwanza kufanyika na pia uliangalia kiwango cha kujua kusoma kupitia mitandao.

Mapigano yasitishwa mji mkuu Sana’a na sasa yahamia viungani

Nchini Yemen baada ya mfululizo wa mashambulizi ya anga na ardhini kuanzia mwishoni mwa wiki kwenye mji mkuu Sana’a, hatimaye hii leo mashambulizi yamekoma na hivyo wananchi kuweza kuibuka kutoka kwenye makazi yao ili kupata huduma.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka mjini humo, mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen, Jamie McGoldrick amesema siku tano za machungu zimekoma baada ya kusabaisha vifo vya watu wapatao 125 na mamia ya majeruhi.