Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

CSW70

Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani
Mkutano wa 70 - CSW70

Kuanzia tarehe 9 hadi 19 Machi 2026, macho na masikio yataelekezwa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambako kutafanyika Mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW70.

Hili ni jukwaa kubwa zaidi la kila mwaka la Umoja wa Mataifa linalojikita katika usawa wa kijinsia na haki za wanawake. Kinachotokea katika CSW huwa na mchango kwenye sheria, sera, ufadhili na uwajibikaji katika nchi mbalimbali na kwa vizazi tofauti.

Kinachomulikwa mwaka huu ni:  Haki, Sheria na Hatua kwa Wanawake na Wasichana wote, ikienda sambamba na kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya wanawake duniani Machi 8.

UN News

Mataifa yaondokane na mila potofu ili wanawake na wasichana wawe huru - Salome Gatakaa 

FODDAJ ambalo ni Jukwaa la Maendeleo ya Wanawake, Demokrasia na Haki, nchini Kenya ni shirika la kiraia ambalo mwaka huu kwa mara nyingine lilishiriki mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani CSW70 uliofanyika mwezi Machi mwaka huu kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Baada ya kushriki vikao mmoja wa viongozi wa shirika hilo amezungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa na ndio msingi wa mahojiano haya.

UN News

Kubadili mtazamo wa jamii ya Samburu kuhusu haki za wanawake ni mtihani tunaoukabili kila siku: Lemachokoti

Kwa wanawake na wasichana wa jamii ya Kaunti ya Samburu Kaskazini mwa Kenya kutorithi chochote katika jamii imekuwa kama ada, kwani mila na utamaduni uliokita mizizi miaka nenda miaka rudi ni chachu kubwa ya kuwakosesha haki. Sasa mambo yameanza kubadilika ingawa changamoto hazikosekani kama anavyoeleza Severina Lemachokoti kutoka asasi ya kiraia ya Naretu Girls and Women Empowerment Programme katika kaunti hiyo, alipozungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii kandoni mwa mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani CSW70 uliokunja jamvi mwezi uliopita. Severina naanza kwa kufafanua wanachofanya kuhakikisha wanawake na wasichana Samburu wanapata haki.