Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

CSW70

Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani
Mkutano wa 70 - CSW70

Kuanzia tarehe 9 hadi 19 Machi 2026, macho na masikio yataelekezwa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambako kutafanyika Mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW70.

Hili ni jukwaa kubwa zaidi la kila mwaka la Umoja wa Mataifa linalojikita katika usawa wa kijinsia na haki za wanawake. Kinachotokea katika CSW huwa na mchango kwenye sheria, sera, ufadhili na uwajibikaji katika nchi mbalimbali na kwa vizazi tofauti.

Kinachomulikwa mwaka huu ni:  Haki, Sheria na Hatua kwa Wanawake na Wasichana wote, ikienda sambamba na kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya wanawake duniani Machi 8.

Wanawake wawili katika mpangilio wa studio, wakiwa wameketi kwenye meza ya duara wakiwa na maikrofoni, wakishiriki katika majadiliano mbele ya mandhari yenye nembo UN .
UN News/Feissal Kirwa

Wavamizi wote waondoke DRC ili sisi ‘wakongomani’ tuendeleze nchi yetu – Bi. Kibuya

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasiaya Congo, DRC, shirika la kiraia la Congo Notre Avenir, yaani kwa kiswahili, Congo Mustakabali wetu linapigania haki ya amani kwa wanawake ili hatimaye waweze kushiriki katika kuendeleza familia zao kwa kushirikiana na familia zao, wakati huu ambapo mapigano mashariki mwa nchi yamesababisha ukatili ikiwemo ubakaji, na hata wanaume kuacha familia zao na kwenda msituni kupigana.

UN News

Tunatoka nje ya mahakama na kufuata wananchi kuwaelimisha – TAWJA

Upatikanaji wa haki hususan kwa wanawake na wasichana hukumbwa na vikwazo lukuki ikiwemo ukosefu wa uelewa wa haki zenyewe. Nchini Tanzania Chama cha Wanawake Majaji, (TAWJA) kimetambua pengo hilo na ndio maana tangu kuanzishwa kwake mwaka 2000 kimekuwa kinachukua hatua kuhakikisha kwamba kabla ya kusaka haki, wanawake na wasichana wanatambua haki zao. Kufahamu nini kinafanyika, Assumpta Massoi wa Idhaa hii mwezi Machi mwaka huu kando ya mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW70 hapa Umoja wa Mataifa, alizungumza na Mwenyekiti wa TAWJA, Barke Sehel ambaye ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa.

UN News

Mataifa yaondokane na mila potofu ili wanawake na wasichana wawe huru - Salome Gatakaa 

FODDAJ ambalo ni Jukwaa la Maendeleo ya Wanawake, Demokrasia na Haki, nchini Kenya ni shirika la kiraia ambalo mwaka huu kwa mara nyingine lilishiriki mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani CSW70 uliofanyika mwezi Machi mwaka huu kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Baada ya kushriki vikao mmoja wa viongozi wa shirika hilo amezungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa na ndio msingi wa mahojiano haya.

UN News

Kubadili mtazamo wa jamii ya Samburu kuhusu haki za wanawake ni mtihani tunaoukabili kila siku: Lemachokoti

Kwa wanawake na wasichana wa jamii ya Kaunti ya Samburu Kaskazini mwa Kenya kutorithi chochote katika jamii imekuwa kama ada, kwani mila na utamaduni uliokita mizizi miaka nenda miaka rudi ni chachu kubwa ya kuwakosesha haki. Sasa mambo yameanza kubadilika ingawa changamoto hazikosekani kama anavyoeleza Severina Lemachokoti kutoka asasi ya kiraia ya Naretu Girls and Women Empowerment Programme katika kaunti hiyo, alipozungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii kandoni mwa mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani CSW70 uliokunja jamvi mwezi uliopita. Severina naanza kwa kufafanua wanachofanya kuhakikisha wanawake na wasichana Samburu wanapata haki.

13 MEI 2026

Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa António Guterres hii leo huko Addis Ababa nchini Ethiopia, wanawake wanaowasili Ulaya kufuatia ukeketaji wa lazima katika nchi zao, na mafunzo ya kutatua migogoro kwa njia mbadala Zanzibar.

Sauti
9'59"
UN News

AfroKids International ni tumaini kwa wanawake wakimbizi barani Ulaya - Farina

Wanawake wengi wahamiaji na wakimbizi kutoka Afrika wanaowasili barani Ulaya wakisaka usalama na maisha bora hujikuta wakikabiliwa na majeraha ya kiwewe, changamoto za lugha na kutengwa kijamii. Nchini Ujerumani, shirika lililoanzishwa na wakimbizi, la AfroKids International, linafanya kazi ya kuwapa matumaini na msaada wanawake hao, hususan manusura wa ukeketaji au FGM.

Sauti
3'19"

04 MEI 2026

Hii leo jaridani tunaangazia ugonjwa unaotokana na virusi vya hantavirus, njaa na afya kwa raia nchini Somalia, na ujumbe wa mshiriki wa mkutano wa CSW70 Hanna Wendot Cheptumo Waziri wa Jinsia, Utamaduni na Maslahi ya Watoto wa Jamhuri ya Kenya kuhusu ukeketaji.

Sauti
9'57"