Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COP26

COP26: 31 Oktoba-12 Novemba 2021 | Glasgow, Uingereza

Kwa takribani miongo mitatu, Umoja wa Mataifa (UN) umekuwa ukileta pamoja kila nchi duniani kwenye mikutano ya ngazi ya juu kuhusu tabianchi, mikutano ikipatiwa jina COP yaani conference of Parties kwa kiswahli wanachama wa mkutano. Tangu wakati huo, mabadiliko ya tabianchi yamebadilika kutoka suala la  pembezoni hadi kipaumbele cha kimataifa.
 
Mwaka huu utakuwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mikutano hiyo, ikipatiwa jina COP26. Uingereza ndio Rais wa mkutano hou wa COP26 na unafanyika Glasgow, Scotland.
Kuelekea COP26, Uingereza inafanya kazi na kila taifa kufikia makubaliano ya jinsi ya kukabili mabadiliko ya tabianchi. Viongozi wa dunia wanawasili Scotland, sambamba na makumi ya maelfu ya washauri, wawakilishi wa serikali, sekta ya biashara, wananchi kwa ajili ya mkutano huo wa siku 12.
Si tu kwamba ni jukumu kubwa, bali pia ni tofaauti na mikutano mingine iliyotangulia ya nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi. Wataalamu wengi wanaamini kuwa COP26 ni dharura ya kipekee.
Ili kupokea taarifa za kila wakati moja moja kwenye akaunti yako ya barua pepe, tafadhali hakikisha  unajisajili hapa kwenye mada kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi

Watu wakiwa katika mto uliofurika Magharibi mwa Haiti baada ya daraja kusombwa na maji kufuatia kimbunga Matthew
MINUSTAH/Logan Abassi

Muda unatutupa mkono kuepuka janga la mabadiliko ya tabianchi:UN Ripoti 

Kupunguzwa kwa muda kwa uzalishaji wa hewa ukaa kulikosababishwa na masharti ya kimataifa ya watu kusalia majumbani wakati wa janga la corona au COVID-19 hakukupunguza kasi ya kuendelea kwa mabadiliko ya tabianchi. Viwango vya gesi chafuzi vimevunja rekodi, na dunia iko njiani  kuelekea hatari joto kali la kupindukia,  imeonya ripoti ya mabadiliko ya tabia nchi iliyotolewa leo na mashirika  mbalimbali.