Tunataka wasichana nchini DRC wasahau machungu ya vita na kuanza maisha mapya: Lydie Mwenge
Pakua
Katika mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ambako miongo ya vita imeacha maelfu ya watoto bila familia, elimu au usalama, Lydie Mbusa Mwenge ameweka maisha yake katika mstari wa mbele wa kupigania haki za wasichana walioathiriwa na vita. Mwenge ni mwanzilishi na mratibu wa shirika la Action Intervention des Femmes Entrepreneurs pour le Développement, linalojikita katika kulinda na kuwawezesha wasichana walio chini ya umri wa miaka 18, hususan wale manusura wa ubakaji, kupoteza familia zao au kulazimika kuishi mitaani. Bi. Lydie Mwenge amezungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii, ungana nao.
Audio Credit
Flora Nducha
Sauti
7'38"