Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maji ni Uti wa mgongo kwa jamii kote duniani - Stephen Tai

Maji ni Uti wa mgongo kwa jamii kote duniani - Stephen Tai

Pakua

Wiki ya Maji ikifikia tamati leo Agosti 28 na maudhui yakiwa Maji kwa ajili ya Hatua kwa Tabianchi, tunabisha hodi kaunti ya Kajiado nchini Kenya kumsikia mtendaji kwenye mradi wa maji wa Kerarapon Water Association  ambalo ni shirika la kijamii linalohusika na maji na mazingira huko kaunti ya Kajiado nchini Kenya. Mtendaji huyo anayeanza kwa kujitambulisha, anazungumza na Kelvin Keitany wa radio washirika Radio Domus nchini Kenya.

Audio Credit
Anold Kayanda/Kevin Keitany
Sauti
5'9"
Photo Credit
UN News