Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNESCO na wadau wanajitahidi kuboresha elimu licha ya mashambulizi dhidi ya elimu katika migogoro.

UNESCO na wadau wanajitahidi kuboresha elimu licha ya mashambulizi dhidi ya elimu katika migogoro.

Pakua

Kama unavyojua, migogoro ya vita, majanga ya tabia nchi, dharura za afya ya umma, na mishtuko ya kiuchumi inaongezeka duniani kote kwa kasi, ugumu, na ukubwa. Mara nyingi dharura hizi hutokea kwa wakati mmoja, kwa mfano, wakati vita vinapoanza katika maeneo ambayo tayari yameathiriwa na majanga ya mabadiliko ya tabianchi. Hali hii inasababisha migogoro tata, iliyo changamana na ya muda mrefu, na athari zake kwenye elimu ni za kutisha. Nafikiri utakubaliana nami kuwa elimu ni mkombozi wa maisha na muhimu kwa kuendeleza maisha wakati wa dharura. Je UNESCO inatatua vipi changamoto hii? Cecili kariuki amezungumza na wataalamu wa elimu nchini Paris, Ufaranza.

Audio Credit
Selina Jerobon/Cecily Kariuki
Audio Duration
4'27"
Photo Credit
United Nations