17 OKTOBA 2023
Pakua
- Asante Leah naazia Mashariki ya Kati ambako mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine yameelezea wasiwasi mkubwa kuhusu hatma raia huko Gaza na Ukingo wa Magaribi yakisistiza fursa ya kufikisha misaada kwa wenye uhitaji likiwemo shirika la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA linalohifadhi wakimbizi wa ndani takribani 400,000 kati ya laki sita sasa katika vituo vyake.
- Katika taarifa nyingine leo UNHCR, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi limetoa tahadhari kuhusu kukithiri kwa ghasia na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu katika majimbo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambazo zimesababisha wimbi jipya la watu kukimbia makazi yao, ndani na nje ya nchi. Licha ya makubaliano ya hivi karibuni ya kusitisha mapigano katika jimbo la Kivu Kaskazini, UNHCR imeripoti kuwa zaidi ya watu 90,000 katika maeneo ya Rutshuru na Masisi wamelazimika kukimbia makazi yao katika wiki za kwanza za Oktoba.
- Nchini Sudan kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, Takriban watu 4,000 wameuawa huku mali na miundombinu ya raia vikiharibiwa vibaya katika vita inavyoendelea Darfur na watu wengine 8,400 wamejeruhiwa, kati ya Aprili 15 na mwisho wa Agosti, huku wengi wao wakilengwa kutokana na sababu za kikabila, hasa eneo la Darfur Magharibi.
- Na mashinani tunakupeleka katika ukanda wa Gaza nchini Palestina kushuhudia jinsi ambavyo watoto na jamii zao wanavyoathirika kufuatia vita kati ya Hamas na Israeli.
Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Audio Credit
Leah Mushi
Audio Duration
12'6"