Ufadhili wa UNCDF umetukwamua sana Kibondo Big Power Group
Pakua
Kibondo Big Power Group (KBPG) ni ushirika wa kilimo mkoani Kigoma, kaskazini magharibi mwa Tanzania. Shirika la mitaji la Umoja wa Mataifa, UNCDF lilisaidia KBPG kwa msaada wa kifedha ambao ulitumika kupanua shughuli zake kwa kufanya shughuli zifuatazo: kuchimba kisima cha maji mita 100, ununuzi wa pampu ya maji ya jua na ujenzi wa ghala na nyumba za kukausha jua za mihogo na chanja na mtaji wa kufanyia kazi. Hamad Rashid wa redio washirika Hamad Rashid wa redio washirika wa Redio washirika wetu MVIWATA FM ya mkoani Morogoro, Tanzania anasimulia zaidi.
Audio Credit
Assumpta Massoi/ Hamad Rashid
Audio Duration
3'52"