Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Changamoto moja kubwa ya kutimiza SDGs ni vijana hawana taarifa za kutosha – Paul Siniga

Changamoto moja kubwa ya kutimiza SDGs ni vijana hawana taarifa za kutosha – Paul Siniga

Pakua

Changamoto moja kubwa ya kutimiza SDGs ni vijana hawana taarifa za kutosha – Paul Siniga 

Mkutano wa 26 wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya madola, CHOGM, unaendelea katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali ambapo leo ni siku ya kwanza ya mkutano wa ngazi za juu. Kandoni mwa mkutano huu, imefanyika mikutano mingine ikijadili mambo kadha yakiwemo Malengo ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu, SDGs. Kijana Paul Peter Siniga yeye akiwa ni Balozi wa SDGs kupitia Umoja wa Mataifa Tanzania, amehudhuria mkutano wa vijana wa jumuiya ya madola ikiwa ni sehemu ya kupeleka ujumbe kwa viongozi hao. Paul anaanza kwa kueleza changamoto ya utimizaji wa malengo haya kwa kundi la vijana. 
 

Audio Credit
Anold Kayanda/ Paul Siniga
Audio Duration
3'44"
Photo Credit
UN/Tanzania