Tunatuma salamu za sikukuu kwa raia wa CAR na tunawatakia mwaka mpya wenye amani - TANBAT 5
Pakua
Katika kuelekea kuukamilisha mwaka 2021 na kuingia katika mwaka mpya wa 2022, Walinda amani wa Kikosi cha 5 cha Tanzania kinacholinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, TANBAT 5 wametuma salamu za kuwatakia msimu wa sikukuu za Krismasi na mwisho wa mwaka raia wanaowalinda. Kupitia taarifa hii iliyoandaliwa na Kapteni Asia Hussein ambaye ni Afisa Habari wa kikosi hicho, anayeanza kutuma salamu ni Luteni Philipo Denis Msaki anayesimamia ukuzaji uhusiano kati ya vikosi, jamii pamoja na asasi za kiraia.
Audio Credit
Assumpta Massoi/ Kapteni Asia Hussein
Audio Duration
2'17"