Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Barua mahsusi ya watoto kwa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Barua mahsusi ya watoto kwa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Pakua

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ambalo limetimiza miaka 75 mwezi huu, kwa miaka yote hiyo tangu mwaka 1946 limekuwa likitoa msaada kwa watoto kote ulimwenguni wakiwemo watoto wa Tanzania. Katika kuadhimisha kumbukumbu hii ya miaka 75, watoto kadhaa wa Tanzania wamemwandikia barua Rais wao, Samia Suluhu Hassan kuzungumzia changamoto zinazowakabili. Kwa ajili ya uwakilishi tu, barua hiyo inasomwa na mtoto Tumaini George akisaidiwa na Mwanaharakati wa masuala ya vijana Meena Ally, pamoja na mshairi maarufu nchini humo, Mrisho Mpoto.

Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
2'33"
Photo Credit
UN Women Tanzania/Deepika Nath