14 Desemba 2021
Pakua
Hujambo na karibu kusikiliza jarida msomaji wako ni Flora Nducha anayekuletea mambo kadha wa kadha ikiwemo
Ripoti inayoonesha kuongeza kwa njaa barani Afrika huku ukanda wa Afrika Mashariki ukiongoza kwa asilimia 44.
Wakimbizi wa DRC walioko nchini Uganda wameanza kurejea makwao kwa hiyari.
Na ushirikiano kati ya vyombo vya usalama ikiwemo polisi na FRDC ambalo ni Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na vikosi vya walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu chini ya Mwavuli wa MONUSCO, umeendelea kuzaa matunda kwa kuwahakikishia usalama wananchi wa maeneo ya mashariki mwa DRC.
Audio Credit
Flora Nducha
Audio Duration
13'9"