walinda amani wa Tanzania nchini CAR watoa msaada wa Madarasa na madawati
Mbali na jukumu la ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya Africa ya Kati CAR, kikosi cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania TANBAT 4 kinachohudumu chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa ujulikanao kama MINUSCA nchini humo , kimeweka mikakati ya kusaidia na kuinua wananchi wa CAR kielimu kupitia shughuli mbalimbali.
Luteni Noela Julius Nyaisangah afisa habrari wa kisoki hicho anafafanua zaidi katika taarifa hii
Natsss…..
Katika mkoa wa wa Mambere Kadei wilaya ya Berberati, sambamba na kutoa ulinzi kwa wananchi TANBAT 4 imekuwa mdau mkubwa wa kusaidia wananchi katika shughuli za kijamii na hivi karibuni wamejenga na kukabidhi vyumba viwili vya madarasa na vifaa vya kufundishia ikiwemo ubao kwa kila darasa na madawati 100.
Vifaa hivyo na madarasa vimekabidhiwa katika shule ya msingi ya kikatoliki ya Secret Heart of Jesus mkoani humo.
TANBAT4 inasema kukamilika kwa madarasa hayo kama sehemu ya maendeleo ya miundombinu nchini CAR yatasaidia shule kuongeza wanafunzi 100 zaidi kwa kila muhula.
Hafla ya kukabidhi madarasa hayo na vifaa ilihudhuriwa na Kamanda wa kikosi cha MINUSCA Luteni Jenerali Daniel Sidiki Traore, Balozi wa Tanzania nchini CAR Luteni Jenerali mstaafu Paul Ignace Mella, Askofu wa Dayosisi ya Berberati, askofu Dennis Kofi Agbenyadzi pamoja na mamlaka za utawala wa mkoa wa Mambere Kadei.
Kamanda kikosi wa MINUSCA aliwapongeza TANBAT4 kwa juhudi zao kwenye kufanikisha ujenzi huo
Naye Balozi wa Tanzania Luteni Jenerali mstaafu Paul Ignace Mella aliongezea kwa kusema
Mwasham Askofu pamoja na mamlaka za utawala wa mkoa wa Mambere Kadei walitoa shukrani zao za dhati kwa TANBAT4 na MINUSCA kwa ujumla kwa mchango wao wa kuinua elimu nchini CAR.