Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Waganda wahaha kukabiliana na athari za mafuriko na COVID-19

Waganda wahaha kukabiliana na athari za mafuriko na COVID-19

Pakua

Majanga asili yametishia juhudi za kufikia malengo ya maendeleo endelevu au SDGs katika nchi zote duniani. Uganda ni miongoni mwa nchi ambazo mwaka huu na mwaka jana 2020 zimeathiriwa moja kwa moja na mlipuko wa COVID-19 na kuongeza chumvi kwenye kidonda cha mafuriko makubwa kihistoria. 

Licha ya changamoto hizo, serikali inawatia moyo wananchi kufanya kazi kwa bidii na kwa busara ili kudhibiti madhara ya majanga haya hasa jamii za ziwani zinazikabiliwa zaidi na majanga hayo mawili wakati mmoja. Makala iliyoandaliwa na John Kibego ina maelezo zaidi.

Audio Credit
Leah Mushi/John Kibego
Audio Duration
3'43"
Photo Credit
UN/ John Kibego