Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano la Mbunge Neema Lugangira kutoka Tanzania kuhusu nafasi ya mbunge kwa umma

Mahojiano la Mbunge Neema Lugangira kutoka Tanzania kuhusu nafasi ya mbunge kwa umma

Pakua

Uwepo wa wabunge wenye nguvu ni msingi imara wa Demokrasia kwani wawakilisha hao wa wananchi wanakuwa na uwezo wa kupitisha sheria, kutenga fedha kwenda kufanya kazi ya utekelezaji wa sheria na sera walizozipitisha na kuwajibisha serikali iwapo haijatenda yale wananchi wanayakusudia kwakuzingatia makundi yote kwenye jamii hususan walioko kwenye mazingira magumu. 

Wabunge pia wanajukumu la kuunganisha masuala ya nchi zao na masuala ya kimataifa na hivyo hupitia na kupitisha mikataba na maadhimio ili kufanya dunia iwe mahali salama na yenye kuwanufaisha wanadamu wote.

Kuelekea siku ya kimataifa ya Mabunge 30 Juni, Leah Mushi amefanya mahojiano na mbunge wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, kuhusu nafasi ya wabunge katika kuhakikisha usalama wa wananchi wao hususani wakati huu dunia ikipambana na janga la corona au COVID19. kwanza anaanza kwa kujitambulisha 
 

Audio Credit
Leah Mushi/Neema Lugangira
Audio Duration
8'51"
Photo Credit
UN News