Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

18 Januari 2021

18 Januari 2021

Pakua

Hii leo Jumatatu ni mada kwa kina tunapiga kambi Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC ambako walinda amani kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO wanafundisha wakazi masuala ya TEHAMA, yaani teknolojia ya habari na mawasiliano. Mwenyeji wetu ni Luteni Issa Mwakalambo. Tuna pia  Habari kwa Ufupi tukimulika COVID-19, Darfur Sudan na Uganda. Mashinani tunakwenda Rwanda. Karibu msomaji wako leo ni Flora Nducha.

Audio Credit
FLORA NDUCHA
Audio Duration
11'54"