Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

13 OKTOBA 2020

13 OKTOBA 2020

Pakua

Katika jarida la habari la Umoja wa Mataifa  hii leo, Flora Nducha anakuletea

-Katika siku ya kimataifa ya kupunguzahatari za majanga Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa antonio Guterres  ameonya kwamba bila udhibiti mzuri wa hatari za majanga , hali ambayo ni mbaya itazidi kubwa mbaya zaidi

-Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya FAO, IFAD, WHO na ILO leo katika taarifa yao ya pamoja yameonya kwamba COVID-19 mbali ya kuathiri afya inaathiri maisha ya watu na mifumo ya chakula hivyo hatua zichukuliwe haraka kunusuru janga zaidi

-Shujaa wa elimu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, mwalimu kutoka Uturuki anasema pamoja na kukatishwa tamaa na janga la COVID-19 wanafunzi wake ambao ni watoto wakimbizi kutoka Syria walimpa nguvu ya kuendfelea kufundisha

-Makala yetu leo inatupeleka Kilimanjaro Tanzania kwa mama mkulima wa pilipili  kupitia msaada wa shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP

-Na mashinani tunakwenda Kenya kwa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani UNFPA, ambapo utamsikia binti  akieleza changamoto za mbimba za utotoni

Audio Credit
UN News/Flora Nducha
Audio Duration
11'42"