Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

06 Agosti 2020

06 Agosti 2020

Pakua
Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Assumpta Massoi 
- Shirika la  mpango wa chakula duniani   WFP wajitosa kuisaidia Lebanon kwani bila bandari ya Beirut, hali itakuwa mbaya zaidi Lebanon
 - Ikiwa leo ni miaka 75 tangu tukio bomu  la Hiroshima nchini Japan, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema njia pekee ya kuondokana na tishio la nyuklia ni kutokomeza silaha za nyuklia.
- Wanawake wafungwa katika gereza la Bimbo wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, Bangui watanufaika na mradi wa ujumuishwaji katika jamii unaotekelezwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu nchini  humo, MINUSCA. 

-Na leo kwenye Makala tunakwenda Uganda ambako kilimo cha pilipili kimegeuka lulu kwa mstaafu ambaye awali alilima zaidi mahindi na maharage.

-Na kwenye  mashinani leo  tunakwenda Burundi kusikia jinsi shirika la Cartedo linajengea uwezo vijana kuhimili maisha hata wakati wa majanga, Karibu!

 

 

 

 

 

 

 

 

 
Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
11'46"