Bado kuna changamoto lakini umuhimu wa huduma za wakunga ni mkubwa
Pakua
Hii leo dunia ikiadhimisha siku ya wakunga duniani, wananchi katika mataifa mbalimbali wameendelea kuhamasishwa kuzitumia huduma zinazotolewa na wakunga wataalamu ili kupunguza vifo vya watoto na akina mama wakati wa kujifungua na hata baada ya hapo wakati wa makuzi ya mtoto. Devotha Songorwa wa redio washirika KidsTime FM amezunguza na baadhi ya wananchi pamoja na wahudumu wa afya mkoani Dodoma nchini Tanzania kuhusu umuhimu na changamoto za wakunga nchini humo.
Audio Credit
Devotha Songorwa
Audio Duration
3'4"