Jumuiya ya wanakiswahili ulimwenguni na duniani kote imehuzunika sana
Miongoni mwao ni Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili huko Zanzibar BAKIZA. "Profesa Ken Walibora ni Mtaalamu ni Mwandishi wa habari ni mwandishi wa vitabu ni Mwalimu lakini ni mwanafastafa muhimu katika taaluma ya lugha ya kiswahili.Alikua tayari kuwakosoa baadhi ya watu kwa kuandika makala mbalimbali kwa kupitia magazeti na hasa gazeti la Taifa leo linalotoka kule Kenya. Lakini pia alikua tayari kuandika kazi za fasihi katika njia tofauti. Kitabu chake kimoja chake ambacho ni msana ni Siku Njema A good day kimetafsiriwa kwa lugha ya kingereza na kifaransa ni riwaya nzuri ambayo inaelezea mambo mengi na muhimu ya kimaisha .Jumuia ya wanakiswahili ulimwenguni na duniani kote imehuzunika sana."
Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi wa Baraza la Kiswahili Tanzania, BAKITA naye akafunguka, "Kikubwa zaidi ambacho Profesa Ken Walibora tunaweza tukamkumbuka ni pale ambapo alijaribu kwa kushirikiana na wenzewe kuandika Islahi mbalimbali katika programu ya Microsoft na Google za kiswahili. Mwafrika wa mashariki mwenzetu ambaye alidhubutu na kujaribu kuingiza hizo isilahi za komputer katika mzuguko wa matumizi yake ya kawaida
Kwa hivyo Kifo cha Ken Walibora sio tu kwamba kimeigusa familia mbali pia kimewajusa familia ya waswahili wote waliofundishwa naye,Vyoo amabayo amehudhuria hata Marekani,Nchi mbalimbali,Kenya alikofanya kazi kama mwanahabari lakini pia amefanya kazi kubwa ya kuandika vitabu ambavyo ameacha kama kumbukumbu katika uga huu wa lugha . Hivyo ni vitu ambavyo sitaweza kumsahau Profesa Ken Walibora."
Leonard Mambo Mbotela, mtangazaji nguli wa siku nyingi nchini Kenya, alikuwa rafiki wa karibu na mwendazake Ken ambapo akihojiwa na mwandishi wetu wa Nairobi, Kenya, Jason Nyakundi, kuhusu kifo cha Ken, anasema,,
(Sauti ya Leonard Mambo Mbotela)
Na vipi kuhusu kitabu ambacho Profesa Ken alikuwa anaandaa kuhusu Mambo Mbotela?
(Sauti ya Leonard Mambo Mbotela)
"Alikuja kwangu ananiambia Bwana Mambo wewe ni mtangazaji mashuhuri mwanahabari mashuhuri waonaje kama tukija na kitabu kuhusu maisha yako?Nikamwambie Ken, hilo ni wazo nzuri sana niko tayari endelea.Nilipomjibu naama hiyo tukapanga basi akaja hapa nyumbani kwangu Langata akanihoji na kupiga picha na kadhalika .Akaniambia sasa anaenda kuandika hicho kitabu Kabla hajafa akanipigia simu na akaniambia naja nyumbani turekebishe mawili matatu na kweli akaja hapa nyumbani tukakaa wiki tatu zilizopita tu tukaskizana na akatoka akashika njia akaenda. Akaniambia usijali ntakupigia tutapangapanga Mwezi wa May Mungu akipenda tutalaunch kitabu. Hivyo ndivyo nilivyo kuwa na mpaka leo hii Kitabu hizo alikiachia msaidizi wake ambaye amenipigia simu leo leo tu akiniambia kwamba Ken ametuwacha lakini Kitabu kitaendelea na tutafanya lauch mwezi huu wa tano."