Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

16 APRILI 2020

16 APRILI 2020

Pakua

Miongoni wa habari ambazo Flora Nducha anakuletea katika Jarida la Umoja wa Mataifa hii leo

- Ubaguzi wa rangi, chuki dhidi ya wageni na hali ya kutovumiliana vimeongezeka wakati huu wa mlipuko wa virusi vya Corona au COVID-19 kwa mujibu wa mtaalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Tendayi Achiume

-Huko Congo DRC visa vipya vya Ebola vimeripotiwa huku taifa hilo la maziwa makuu likiendelea kukabiliana na majanga mengine kama COVID-19,utapiamlo na vita limesema shirika la afya duniani WHO.

-Nchini Kenya mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF wa imarisha afya ya mama na mtoto waleta nuru kwa maisha ya maelfu ya watu

-Makala yetu inatupeleka Tanzania kukutana na mwanamke mjasiriamali na mpambanaji anayeendesha bodaboda kukidhi mahitaji ya familia yake

-Na mashinani tunabisha hodi Kenya kwa mwalimu anayetumia mbinu bunifu kuhakikisha wanafunzi wake wanasoma wakati huu wa COVID-19

Audio Credit
UN News/Flora Nducha
Audio Duration
12'32"