Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuna haja ya kuwekeza kuimarisha sekta ya wahudumu wa afya-WHO

Kuna haja ya kuwekeza kuimarisha sekta ya wahudumu wa afya-WHO

Pakua

Mlipuko wa virusi vya Corona COVID-19 unadhidhirisa haja ya kuimarisha sekta ya wahudumu wa afya kote duniani , kwa mujibu wa ripoti mpya ya “hali ya wauguzi duniani 2020.”Flora Nducha na taarifa zaidi
(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)
Ripoti hiyo iliyotolewa leo inatoa mtazamo wa kina kuhusu kundi kubwa la wafanyakazi wa huduma za afya.
Pia ripoti hiyo imebaini mapengo makubwa yaliyoko katika kundi hilo la wauguzi na maeneo ya kuyapa kipaumbele kama uwekezaji wa elimu kwa wauguzi, ajira na uongozi kuweza kuimarisha wauguzi kote duniani ili kuboresha afya kwa wote.
Waugunzi ni zaidi ya nusu ya wahudumu wote wa afya kwa mujibu wa ripoti hiyo na wanatoa huduma muhimu katika mfumo mzima wa afya.
“Kihistoria na hata ilivyo sasa wauguzi wako msitari wa mbele kupambana na milipuko ya magonjwa ambayo inatishia afya kote ulimwenguni. Duniani kote wanadhihirisha huruma yao, uhodari na ujasiri wakati wa napopambana na janga la COVID-19..”
Akisisitiza umuhimu wa kundi hili la wahudumu wa afya mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani WHO, Dkt. Tedross Adhamon amesema”Wauguzi ni uti wa mgongo wa mfumo wowote wa afya. Leo wauguzi wengi wanajikuta wako msitari wa mbele katika mapambano dhidi ya COVID-19. Na ripoti hiini kumbusho la jukumu muhimu wanalolifanya na kusisitiza kuhakikisha kwamba wanapata msaada wanaouhitaji kuhakikisha dunia inakuwa na afya.”
Naye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiunga mkono hoja hiyo ya umuhimu wa wauguzi amesema 
 
(SAUTI YA ANTONIO GUTERRES- ARNOLD)
“wauguzi hubeba baadhi ya mizigo mkubwa kabisa ya huduma za afya. Wauguzi hufanya kazi ngumu na kwa saa nyingi, huku wakihatarisha kuumia, maambukizi na mzigo wa afya ya akili ambao unaambatana na kazi hiyo inayotia kiwewe. Mara nyingi hutoa faraja wakati wa mwisho wa maisha.”
 
Ripoti hiyo iliyoandaliwa kwa pamoja na WHO kwa kushirikiana na baraza la kimataifa la wauguzi (ICN) na Nursing Now imeonyesha kwamba leo hii duniani kote kuna wauguzi takriban milioni 28 na zaidi ya asilimia 80 ya wauguzi wote duniani wanafanyakazi katika maeneo yaliyo na nusu ya watu wote wa dunia
 
Ili kuepuka pengo la kimataifa la wauguzi ripoti inakadiria kwamba nchi zinazokabiliwa na uhaba wa wauguzi zinatakiwa kuongeza idadi ya wauguzi wanaohitimu kwa wastani wa asilimia 8 kwa mwaka sambamba na kuimarisha uwezo wa kuajiriwa na kusalia kwenye mifumo ya afya. 

Ujumbe wa ripoti hiyo uko bayana “serikali zinahitaji kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika mchakato wa kusomesha wauguzi , kuunda ajira za wauguzi na uongozi. Bila wauguzi, wakunga na wahudumu wengine wa afya nchi haziwezi kushinda vita dhidi ya magonjwa ya milipuko au kufikia huduma za afya kwa wote na malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.

Audio Credit
Assumpta Massoi/ Flora Nducha
Audio Duration
2'49"
Photo Credit
© UNICEF/Thomas Nybo