Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COVID-19: Mradi wa UN-Habitat wafanikisha unawaji mikono Mathare, Kenya

COVID-19: Mradi wa UN-Habitat wafanikisha unawaji mikono Mathare, Kenya

Pakua

Shirika la makazi la Umoja wa Mataifa, UN-Habitat kwa kushirikiana na kituo cha mazingira cha vijana eneo la Mathare jijini Nairobi, Kenya, au  Mathare Environmental One Stop Youth Centre wameungana kwa ajili ya kutoa huduma ya maji safi ya kunawa mikono kwa wakazi 50,000 wa kijiji cha Mlango Kubwa katika mtaa wa Mathare ulioko kwenye mji mkuu wa Kenya, Nairobi. Taarifa kamili na Grace Kaneiya.
(Taarifa ya Grace)
Video ya UN-Habitat inaonesha wakazi wa Kijiji cha Mlango Kubwa kwenye mtaa wa Mathare katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, wakiendelea na shughuli za kila siku. 
Msongamano wa watu na ukosefu wa maji ya kujisafi huenda vikahatarisha wakazi wa mitaa duni kuambukizwa virusi vya corona.
Lakini maradi huu wa pamoja ni  hatua ya kulinda watu hao ambao kwa kawaida husaka maji kwenye maeneo ya umma. Maji hayo yanasafirishwa kwa kutumia mikokoteni yakiwa kwenye mitungi ya plastiki.
Kituo hiki kwa ushirikiano na UN-Habitat ni cha kwanza cha aina hiyo kwa ajili ya kunawa mikono  ambapo mradi huo unatarajiwa kuanzishwa katika maeneo mengine ya mitaa ya mabanda ya Mathare.
Kunawa mikono kwa maji yanayotiririka na sabuni ni moja ya mapendekezo a wataalamu wa afya kama moja wapo ya hatua za kudhibiti kusambaa kwa virusi vya corona.
Hatua hii inakuja wakati huu ambapo hadi Jumanne wiki hii Kenya imeripoti wagonjwa 25 wa virusi vya corona, COVID-19 waliothibitishwa.

Audio Credit
Assumpta Massoi/ Grace Kaneiya
Audio Duration
1'26"
Photo Credit
© Julius Mwelu/ UN-Habitat