Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

TB ikichanganyika na COVID-19 ni janga juu ya janga

TB ikichanganyika na COVID-19 ni janga juu ya janga

Pakua

Ugonjwa wa Kifua Kikuu au TB, bado umesalia kuwa miongoni mwa magonjwa hatari zaidi duniani. Zaidi ya watu 4000 hupoteza maisha yao  kila siku kutokana na ugonjwa TB huku 30,000 wakiwa wanapata maambukizi ya ugonjwa huu unaoweza kuzuiwa na kutibiwa. Gonjwa hili linasalia kuwa tishio wakati huu ambapo kumeibuka virusi vya ugonjwa wa Corona au COVID-19 ambao nao umetikisa dunia ukisambaa katika mataifa 189 na ukiwa umesababisha vifo vya watu zaidi ya 14,500 tangu kubainika mwezi Desemba mwaka jana. Ugonjwa huu nao unaathiri mapafu na ni kwa mantiki hiyo katika maadhimisho ya siku ya kutokomeza TB duniani hii leo tunaangazia hatari ya COVID-19 kwa mtu aliyeugua TB na mwandishi wetu wa Nairobi, Kenya amezungumza na Daktari Jeremiah Jakaya kufahamu hilo naye hakusita kwa kuanza kuchambua katika makala hii

Audio Credit
Jason Nyakundi
Audio Duration
4'
Photo Credit
© UNICEF/Ilvy Njiokiktjien