Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwanamke Mjasiriamali Ester Damiani anayeponda mawe kuwa kokoto,Tanzania

Mwanamke Mjasiriamali Ester Damiani anayeponda mawe kuwa kokoto,Tanzania

Pakua

Wakati tukielekea kuadhimisha siku ya kimataifa ya wanawake  tarehe 8 ya mwezi huu ambapo kaulimbiu yaa mwaka huu inaangazia kizazi cha usawa, yaani kizazi ambacho mwanamke habaki nyuma.

 

Licha ya wanawake wengi kuathiriwa na imani ya kuwa  kuna kazi za kiume na za kike wapo baadhi ambao wameamua kuithibitishia jamii kuwa dhana hiyo ni potofu. Mathalani Ester Damiani mwenyeji wa Kakonko mkoani Kigoma ambaye kwa sasa yuko wilayani kahama mkoani shinyanga akitafuta riziki, kwa miaka 10 anajishughulisha na ujasiliamali wa kuponda mawe kuwa kokoto na kazi hii anasema anaipenda sana kama alivyozungumza na PAULINA MPIWA wa radio washirika Huheso Fm ya wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Audio Credit
GRACE KANEYA
Audio Duration
6'17"
Photo Credit
UN News Kiswahili